Jifunze Kiswahili: Maana ya neno "NDUI" | | Habari za UN
Na tugeukie katika kujifunza lugha adhimu ya Kiswahili na leo tunapata ufafanuzi wa neno "NDUI" kutoka kwa mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA.
Ndui ni ugonjwa ambao sasa hivi watu wengi hawaufahamu. Huu ni ugonjwa kama vile tetekuwanga, ambao unaenezwa na virusi vinavyoshambulia mwili aghalabu huwacha madoadoa meusi kwenye ngozi baada ya kupona. Ni aina ya upele ambao unampata mtu na ugonjwa huo unaambukizwa na virusi. Na huu ni ugonjwa ambao ulikuweko sana miaka ya nyuma. Sasa hivi ni nadra kutokana na chanjo mbalimbali ambazo watu wanazipata. Lakini pia inaweza kutokana na mazingira na ukomavu wa sayansi na teknolojia katika kuthibiti virusi hivi.