×

We use cookies to help make LingQ better. By visiting the site, you agree to our cookie policy.


image

Habari za UN, WHO: Mwongozo mpya kusaidia kupunguza vifo vya watumiaji pikipiki | | Habari za UN

WHO: Mwongozo mpya kusaidia kupunguza vifo vya watumiaji pikipiki | | Habari za UN

Hii leo shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO kwa kutambua majeraha ya kichwa ndio sababu inayoongoza vifo vya waendesha pikipiki duniani, limezindua mwongozo mpya utakaowezesha mamlaka kuongeza matumizi ya helmeti kwa waendeshaji na watumiaji wa pikipiki.

Mwongozo huo umepitishwa hii leo huko Mumbai nchini India kunakofanyika mkutano wa siku mbili wa kanda ya Asia kuhusu Usalama Barabarani Duniani ukijikita katika matumizi ya helmeti bora kwa ajili ya kupunguza vifo na majeraha.

WHO inasema mwongozo utasaidia mamlaka kutunga sheria, kanuni na hatua zinazotakiwa ili kuongeza usalama, ubora wa helmeti na hatimaye kuokoa maisha.

Taarifa ya WHO iliyochapishwa leo inasema matumizi ya helmeti zenye ubora hupunguza hatari ya vifo mara sita zaidi ilhali hatari ya ubongo kuathirika hupungua kwa hadi asilimia 74.

Ukosefu wa helmeti bora, salama na zenye gharama nafuu, vinatajwa kuwa sababu za watu kutotumia helmeti, halikdhalika ukosefu wa helmeti za watoto, kutokusimamiwa kwa sheria zilizoko na joto.

WHO inasema helmeti ambayo haijavaliwa na kufungwa vizuri huongeza pia hatari ya kifo na majeraha iwapo ajali itatokea.

Ingawa hivyo bado matumizi ya helmeti kwenye nchi nyingi za kipato cha chini na kati ni kidogo licha ya ongezeko la kasi la pikipiki.

Dkt. Matts-Ake Belin, kiongozi wa Muongo wa Umoja wa Mataifa wa usalama barabarani mwaka 2021 hadi 2030 anasema kwa kuwa pikipiki zinaongezeka kwa kasi kubwa kwenye nchi za kipato cha chini na cha kati, hatua za dharura zinahitajika kuondokana na vifo na majeraha katika miaka ijayo.

Dkt. Belin anasisitiza kuwa mamlaka lazima ziweke sheria, mifumo na hatua za kuchagiza uwepo na uvaaji wa helmeti bora na mwongozo uliozinduliwa leo umetaja viwango vya ubora.

Mwongozo utasaidia kuanzisha mfumo wa kuchagiza matumizi ya helmeti, ikiwemo sheria ya kimataifa kuhusu helmeti, viwango vya ubora, usimamizi wa sheria na elimu.

WHO inasema mfumo wa matumizi ya helmeti zenye ubora na salama umesaidia Norway na Sweden kupunguza kwa kiasi kikubwa vifo na majeraha yatokanayo na ajali za pikipiki.

WHO: Mwongozo mpya kusaidia kupunguza vifo vya watumiaji pikipiki | | Habari za UN WHO: New guidelines to help reduce the death of motorcycle users | | UN news OMS: Nuevas directrices para ayudar a reducir la muerte de usuarios de motocicletas | | noticias de la ONU OMS : De nouvelles lignes directrices pour contribuer à réduire le nombre de décès chez les motocyclistes | | Actualités de l'ONU OMS: Novas diretrizes para ajudar a reduzir a morte de usuários de motocicleta | | notícias da ONU

Hii leo shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO kwa kutambua majeraha ya kichwa ndio sababu inayoongoza vifo vya waendesha pikipiki duniani, limezindua mwongozo mpya utakaowezesha mamlaka kuongeza matumizi ya helmeti kwa waendeshaji na watumiaji wa pikipiki. Aujourd'hui, l'Organisation mondiale de la santé des Nations Unies (OMS), reconnaissant que les traumatismes crâniens sont la principale cause de décès des motocyclistes dans le monde, a publié une nouvelle directive qui permettra aux autorités d'augmenter l'utilisation du casque pour les motocyclistes et les utilisateurs.

Mwongozo huo umepitishwa hii leo huko Mumbai nchini India kunakofanyika mkutano wa siku mbili wa kanda ya Asia kuhusu Usalama Barabarani Duniani ukijikita katika matumizi ya helmeti bora kwa ajili ya kupunguza vifo na majeraha. Le guide a été adopté aujourd'hui à Mumbai, en Inde, où se tient une réunion de deux jours de la région asiatique sur la sécurité routière mondiale, axée sur l'utilisation de meilleurs casques pour réduire les décès et les blessures.

WHO inasema mwongozo utasaidia mamlaka kutunga sheria, kanuni na hatua zinazotakiwa ili kuongeza usalama, ubora wa helmeti na hatimaye kuokoa maisha. L'OMS affirme que ce guide aidera les autorités à promulguer les lois, réglementations et mesures nécessaires pour accroître la sécurité et la qualité des casques et, à terme, sauver des vies.

Taarifa ya WHO iliyochapishwa leo inasema matumizi ya helmeti zenye ubora hupunguza hatari ya vifo mara sita zaidi ilhali hatari ya ubongo kuathirika hupungua kwa hadi asilimia 74.

Ukosefu wa helmeti bora, salama na zenye gharama nafuu, vinatajwa kuwa sababu za watu kutotumia helmeti, halikdhalika ukosefu wa helmeti za watoto, kutokusimamiwa kwa sheria zilizoko na joto.

WHO inasema helmeti ambayo haijavaliwa na kufungwa vizuri huongeza pia hatari ya kifo na majeraha iwapo ajali itatokea.

Ingawa hivyo bado matumizi ya helmeti kwenye nchi nyingi za kipato cha chini na kati ni kidogo licha ya ongezeko la kasi la pikipiki. Cependant, le port du casque reste faible dans de nombreux pays à revenu faible ou intermédiaire, malgré l’essor rapide de la pratique de la moto.

Dkt. Matts-Ake Belin, kiongozi wa Muongo wa Umoja wa Mataifa wa usalama barabarani mwaka 2021 hadi 2030 anasema kwa kuwa pikipiki zinaongezeka kwa kasi kubwa kwenye nchi za kipato cha chini na cha kati, hatua za dharura zinahitajika kuondokana na vifo na majeraha katika miaka ijayo. Matts-Ake Belin, responsable de la Décennie des Nations Unies pour la sécurité routière 2021 à 2030, affirme que puisque le nombre de motocyclettes augmente rapidement dans les pays à revenu faible et intermédiaire, des mesures urgentes sont nécessaires pour éliminer les décès et les blessures dans les années à venir.

Dkt. Belin anasisitiza kuwa mamlaka lazima ziweke sheria, mifumo na hatua za kuchagiza uwepo na uvaaji wa helmeti bora na mwongozo uliozinduliwa leo umetaja viwango vya ubora.

Mwongozo utasaidia kuanzisha mfumo wa kuchagiza matumizi ya helmeti, ikiwemo sheria ya kimataifa kuhusu helmeti, viwango vya ubora, usimamizi wa sheria na elimu. Le guide contribuera à établir un cadre pour façonner l'utilisation des casques, y compris la législation internationale sur les casques, les normes de qualité, l'application de la loi et l'éducation.

WHO inasema mfumo wa matumizi ya helmeti zenye ubora na salama umesaidia Norway na Sweden kupunguza kwa kiasi kikubwa vifo na majeraha yatokanayo na ajali za pikipiki.