×

We use cookies to help make LingQ better. By visiting the site, you agree to our cookie policy.

Habari za UN, Jifunze Kiswahili: Maana ya neno "NDUI" | | H… – Text to read

Habari za UN, Jifunze Kiswahili: Maana ya neno "NDUI" | | Habari za UN

Intermediate 2 Swahili lesson to practice reading

Start learning this lesson now

Jifunze Kiswahili: Maana ya neno "NDUI" | | Habari za UN

Na tugeukie katika kujifunza lugha adhimu ya Kiswahili na leo tunapata ufafanuzi wa neno "NDUI" kutoka kwa mtaalam wetu Onni Sigalla, Mhariri mwandamizi wa Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania, BAKITA.

Ndui ni ugonjwa ambao sasa hivi watu wengi hawaufahamu. Huu ni ugonjwa kama vile tetekuwanga, ambao unaenezwa na virusi vinavyoshambulia mwili aghalabu huwacha madoadoa meusi kwenye ngozi baada ya kupona. Ni aina ya upele ambao unampata mtu na ugonjwa huo unaambukizwa na virusi. Na huu ni ugonjwa ambao ulikuweko sana miaka ya nyuma. Sasa hivi ni nadra kutokana na chanjo mbalimbali ambazo watu wanazipata. Lakini pia inaweza kutokana na mazingira na ukomavu wa sayansi na teknolojia katika kuthibiti virusi hivi.

Learn languages from TV shows, movies, news, articles and more! Try LingQ for FREE