×

Vi använder kakor för att göra LingQ bättre. Genom att besöka sajten, godkänner du vår cookie-policy.


image

Habari za UN, Wakimbizi wa ndani DRC wakabiliwa na vitendo vya ukatili wa kijinsia na kingono | | Habari za UN

Wakimbizi wa ndani DRC wakabiliwa na vitendo vya ukatili wa kijinsia na kingono | | Habari za UN

Mratibu wa masuala ya kibinadamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC Bruno Lemarquis amezungumza na waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi hii leo na kusema vitendo vya ukatili wa kijinsia na kingono dhidi ya wanawake na wasichana kwenye makazi ya wakimbizi wa ndani nchini DRC vimeongezeka kwa asilimia 37 mwaka huu ikilinganishwa na mwaka jana, huku akitaka hatua za haraka zichukuliwe ili kurekebisha kinachoendelea.

Assumpta Massoi amefuatilia na hii hapa taarifa yake.

Katika mkutano wake huo uliomulika hali ya kibinadamu nchini DRC, Bwana Lemarquis ambaye pia ni Naibu Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini DRC amesema mwaka jana pekee kwenye makazi ya wakimbizi katika jimbo la Kivu Kaskazini, kulikuwa na matukio zaidi ya 38,000 ya ukatili wa kingono na kwamba katika miezi mitatu ya mwanzo wa mwaka huu pekee, kumekuweko na ongezeko kwa asilimia 37.

Amesema “wanawake na watoto walio hatarini zaidi ambao wanasaka hifadhi kwenye makazi hayo, wanajikuta wakikabiliwa na ukatili na machungu zaidi na hili halivumiliki.”

Hivyo amesema hatua zaidi zinahitajika kuchukuliwa na serikali pamoja na wadau ili kudhibiti hali hiyo.

Lemarquis amesema ongezeko la wakimbizi wa ndani kwenye makazi linatokana pia na ombwe la ulinzi kwenye maeneo ya kaskazini mwa jimbo la Kivu Kaskazini, Ituri na Kivu Kusini kutokana na vikosi vya usalama kuhamishwa ili kwenda kukabiliana na waasi wa M23.

Amesema baadhi ya makundi yaliyojihami kama vile ADF, Zaire na CODECO yametumia fursa hiyo kushamirisha mashambulizi yao dhidi ya raia hususan Ituri.

Naibu Mwakilishi huyo wa Katibu Mkuu nchini DRC amegusia pia jimbo la Mai-Ndombe lililoko magharibi mwa DRC, ambako amesema ghasia zilizoibuka mwezi Juni mwaka jana zimeendelea na zinasambaa kwenye maeneo ya jirani; na kwamba, kwa kuwa DRC inaelekea kwenye uchaguzi, ni vema kuchukua hatua kudhibiti ili ghasia hizo zisije kuwa chanzo cha janga lingine la kibinadamu nchini humo.

Wakimbizi wa ndani DRC wakabiliwa na vitendo vya ukatili wa kijinsia na kingono | | Habari za UN Interne Flüchtlinge in der Demokratischen Republik Kongo sind mit geschlechtsspezifischer und sexueller Gewalt konfrontiert | UN-Nachrichten Internal refugees in the DRC are facing acts of gender and sexual violence | UN news Los refugiados internos en la República Democrática del Congo se enfrentan a actos de violencia sexual y de género | noticias de la ONU Les réfugiés internes en RDC sont confrontés à des actes de violences sexistes et sexuelles | Actualités de l'ONU Uchodźcy wewnętrzni w DRK spotykają się z aktami przemocy na tle płciowym i seksualnym | Wiadomości ONZ Refugiados internos na RDC enfrentam atos de violência sexual e de gênero | notícias da ONU 刚果民主共和国境内难民面临性别暴力和性暴力行为|联合国新闻

Mratibu wa masuala ya kibinadamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC Bruno Lemarquis amezungumza na waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi hii leo na kusema vitendo vya ukatili wa kijinsia na kingono dhidi ya wanawake na wasichana kwenye makazi ya wakimbizi wa ndani nchini DRC vimeongezeka kwa asilimia 37 mwaka huu ikilinganishwa na mwaka jana, huku akitaka hatua za haraka zichukuliwe ili kurekebisha kinachoendelea. Le coordinateur des affaires humanitaires en République démocratique du Congo, RDC, Bruno Lemarquis, s'est entretenu aujourd'hui avec des journalistes à Genève, en Suisse, et a déclaré que les actes de violence sexiste et sexuelle contre les femmes et les filles dans les refuges de réfugiés internes en RDC ont augmenté de 37. pour cent cette année par rapport à l’année dernière, alors qu’il souhaitait que des mesures immédiates soient prises pour corriger ce qui se passe.

Assumpta Massoi amefuatilia na hii hapa taarifa yake.

Katika mkutano wake huo uliomulika hali ya kibinadamu nchini DRC, Bwana Lemarquis ambaye pia ni Naibu Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini DRC amesema mwaka jana pekee kwenye makazi ya wakimbizi katika jimbo la Kivu Kaskazini, kulikuwa na matukio zaidi ya 38,000 ya ukatili wa kingono na kwamba katika miezi mitatu ya mwanzo wa mwaka huu pekee, kumekuweko na ongezeko kwa asilimia 37. Lors de sa rencontre qui a fait la lumière sur la situation humanitaire en RDC, M. Lemarquis, qui est également le Représentant spécial adjoint du Secrétaire général des Nations Unies en RDC, a déclaré que l'année dernière seulement, dans les camps de réfugiés de la province du Nord-Kivu, il y avait Il y a eu plus de 38 000 incidents de violence et qu'au cours des seuls trois premiers mois de cette année, il y a eu une augmentation de 37 pour cent.

Amesema “wanawake na watoto walio hatarini zaidi ambao wanasaka hifadhi kwenye makazi hayo, wanajikuta wakikabiliwa na ukatili na machungu zaidi na hili halivumiliki.”

Hivyo amesema hatua zaidi zinahitajika kuchukuliwa na serikali pamoja na wadau ili kudhibiti hali hiyo.

Lemarquis amesema ongezeko la wakimbizi wa ndani kwenye makazi linatokana pia na ombwe la ulinzi kwenye maeneo ya kaskazini mwa jimbo la Kivu Kaskazini, Ituri na Kivu Kusini kutokana na vikosi vya usalama kuhamishwa ili kwenda kukabiliana na waasi wa M23.

Amesema baadhi ya makundi yaliyojihami kama vile ADF, Zaire na CODECO yametumia fursa hiyo kushamirisha mashambulizi yao dhidi ya raia hususan Ituri.

Naibu Mwakilishi huyo wa Katibu Mkuu nchini DRC amegusia pia jimbo la Mai-Ndombe lililoko magharibi mwa DRC, ambako amesema ghasia zilizoibuka mwezi Juni mwaka jana zimeendelea na zinasambaa kwenye maeneo ya jirani; na kwamba, kwa kuwa DRC inaelekea kwenye uchaguzi, ni vema kuchukua hatua kudhibiti ili ghasia hizo zisije kuwa chanzo cha janga lingine la kibinadamu nchini humo.