×

Vi använder kakor för att göra LingQ bättre. Genom att besöka sajten, godkänner du vår cookie-policy.


image

Habari za UN, Makundi yenye silaha DRC waweweke chini silaha zao: Keita | | Habari za UN

Makundi yenye silaha DRC waweweke chini silaha zao: Keita | | Habari za UN

Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC Bintou Keita amesema kwamba mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO unasisitiza wito wa Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa makundi yenye silaha yanayoendesha operesheni zao DRC kuweka chini silaha zao mara moja na bila ya masharti yoyote. Mwandishi wetu wa Kinshasa Byobe Malenga na taarifa zaidi.

Bi Bintou Keita, Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu nchini DRC ametoa kauli hiyo wakati wa mkutano na waandishi wa habari wakati akitimisha ziara yake mwishoni mwa wiki katika majimbo matatu ya Mashariki mwa nchi ambapo amesema amehuzunishwa sana na hali ya wakimbizi wa ndani, “Nilikuja kuona kwa uhakika athari za kuzorota kwa hali ya usalama katika maisha ya mamia kwa maelfu ya watu walio katika mazingira magumu, wakiwemo wanawake na watoto. Nimetembelea maeneo ya Bushagara na Mugwera huko Kivu Kaskazini na Kisoge huko Ituri. Nimekutana na wanawake na wanaume walio katika dhiki lakini ambao bado wana matumaini. Wana nia moja tu ya kurejea kwa amani ili warudi majumbani kwao salama. Haya ni matakwa yetu ya pamoja.”

Keita amewataka waasi wa kundi la M23 kuheshimu mkataba wa mwisho wa mkutano mdogo wa kilele uliofanyika mjini Launda nchini Angola ambao unaowataka waasi hao kuondoka na kurejea katika nafasi yao ya awali kwenye Mlima Sabinyo kabla ya Jumanne ya Machi 7 mwaka huu bila masharti kabla ya kutaka mazungumzo yoyote na serikali ya DRC,

“Ninakaribisha hatua ya mpatanishi wa Umoja wa Afrika, Rais wa Angola Joao Lourenço, ambayo imefanya Ijumaa kutolewa ahadi ya M23 ya kusitisha mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuanzia Jumanne tarehe 7 Machi saa 12 Jioni. Ninatoa wito kwa vuguvugu hili la waasi wa M23 kuheshimu bila masharti au kusita, masharti ya tamko la Luanda la Novemba 23, ambalo linadai wajiondoe katika maeneo yanayokaliwa, kusitishwa kwa mapigano yote, kuwaondoa wapiganaji wao na kurudi katika eneo lao la awali kwenye Mlima Sabino “.

Wito huo unakuja wakati waasi wa M23 wakiteka vijiji kadhaa katika maeneo ya Masisi, Rutshuru na Nyiragongo, hali iliyosababisha zaidi ya watu 600,000 kuyahama makazi yao.

Makundi yenye silaha DRC waweweke chini silaha zao: Keita | | Habari za UN Armed groups in the DRC should lay down their weapons: Keita | | UN news Los grupos armados en la República Democrática del Congo deberían deponer las armas: Keita | | noticias de la ONU Les groupes armés en RDC devraient déposer les armes : Keita | | Actualités de l'ONU Grupos armados na RDC devem depor as armas: Keita | | notícias da ONU

Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC Bintou Keita amesema kwamba mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo MONUSCO unasisitiza wito wa Antonio Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa makundi yenye silaha yanayoendesha operesheni zao DRC kuweka chini silaha zao mara moja na bila ya masharti yoyote. The representative of the Secretary General of the United Nations in the Democratic Republic of the Congo, Bintou Keita has said that the United Nations program in the country, MONUSCO, emphasizes the call of Antonio Guterres, the Secretary General of the United Nations for the armed groups conducting their operations in the DRC to lay down their arms immediately and without any conditions. Mwandishi wetu wa Kinshasa Byobe Malenga na taarifa zaidi. Our Kinshasa reporter Byobe Malenga has more information. Notre correspondant à Kinshasa Byobe Malenga a plus d'informations.

Bi Bintou Keita, Mwakilishi Maalum wa Katibu Mkuu nchini DRC ametoa kauli hiyo wakati wa mkutano na waandishi wa habari wakati akitimisha ziara yake mwishoni mwa wiki katika majimbo matatu ya Mashariki mwa nchi ambapo amesema amehuzunishwa sana na hali ya wakimbizi wa ndani, Ms. Bintou Keita, the Special Representative of the Secretary General in the DRC made the statement during a press conference at the end of her visit at the end of the week in three states in the East of the country where she said she was very saddened by the situation of internal refugees. “Nilikuja kuona kwa uhakika athari za kuzorota kwa hali ya usalama katika maisha ya mamia kwa maelfu ya watu walio katika mazingira magumu, wakiwemo wanawake na watoto. Nimetembelea maeneo ya Bushagara na Mugwera huko Kivu Kaskazini na Kisoge huko Ituri. J'ai visité Bushagara et Mugwera au Nord-Kivu et Kisoge en Ituri. Nimekutana na wanawake na wanaume walio katika dhiki lakini ambao bado wana matumaini. J'ai rencontré des femmes et des hommes en détresse mais qui ont encore de l'espoir. Wana nia moja tu ya kurejea kwa amani ili warudi majumbani kwao salama. Haya ni matakwa yetu ya pamoja.”

Keita amewataka waasi wa kundi la M23 kuheshimu mkataba wa mwisho wa mkutano mdogo wa kilele uliofanyika mjini Launda nchini Angola ambao unaowataka waasi hao kuondoka na kurejea katika nafasi yao ya awali kwenye Mlima Sabinyo kabla ya Jumanne ya Machi 7 mwaka huu bila masharti kabla ya kutaka mazungumzo yoyote na serikali ya DRC, Keita a demandé aux rebelles du groupe M23 de respecter l'accord final du mini-sommet tenu à Launda en Angola, qui appelle les rebelles à quitter et à revenir à leur position initiale sur le Mont Sabinyo avant le mardi 7 mars de cette année, sans conditions. avant de demander des négociations au gouvernement de la RDC,

“Ninakaribisha hatua ya mpatanishi wa Umoja wa Afrika, Rais wa Angola Joao Lourenço, ambayo imefanya Ijumaa kutolewa ahadi ya M23 ya kusitisha mapigano mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kuanzia Jumanne tarehe 7 Machi saa 12 Jioni. Ninatoa wito kwa vuguvugu hili la waasi wa M23 kuheshimu bila masharti au kusita, masharti ya tamko la Luanda la Novemba 23, ambalo linadai wajiondoe katika maeneo yanayokaliwa, kusitishwa kwa mapigano yote, kuwaondoa wapiganaji wao na kurudi katika eneo lao la awali kwenye Mlima Sabino “.

Wito huo unakuja wakati waasi wa M23 wakiteka vijiji kadhaa katika maeneo ya Masisi, Rutshuru na Nyiragongo, hali iliyosababisha zaidi ya watu 600,000 kuyahama makazi yao. Cet appel intervient alors que les rebelles du M23 ont capturé plusieurs villages dans les régions de Masisi, Rutshuru et Nyiragongo, une situation qui a poussé plus de 600 000 personnes à quitter leurs foyers.