×

Мы используем cookie-файлы, чтобы сделать работу LingQ лучше. Находясь на нашем сайте, вы соглашаетесь на наши правила обработки файлов «cookie».

Habari za UN, Methali: Aanguae huanguliwa | | Habari za UN – Текст для чтения

Habari za UN, Methali: Aanguae huanguliwa | | Habari za UN

Средний 2 Урок суахили для практики чтения

Начать изучать этот урок прямо сейчас

Methali: Aanguae huanguliwa | | Habari za UN

Na sasa ni wasaa wa kujifunza Kiswahili. Mchambuzi wetu Dkt. Josephat Gitonga, kutoka Kenya ambaye ni mhadhiri katika Chuo Kikuu cha Nairobi kwenye kitivo cha tafsiri na ukalimani anatufafanulia methali isemayo “Aanguae huanguliwa.”

Aanguae huanguliwa. Ni methali iliyo na maana ya msingi kuwa, kuna wanyama ambao hutaga mayai. Mayai haya baadaye huanguliwa baada ya muda fulani wa kutunzwa na kupashwa joto na aliyeyataga. Huyu naye aliyeyataga naye katagwa na kuanguliwa. Ndiyo maana anataga na kuangua. Asingalifanywa na kuanguliwa hangalikuwepo. Inatufunza [methali] kwamba hakuna kinachotokana na ombwe tupu. Kila kitu kina asili yake. Hata kama mtu ana sifa gani, ziwe njema au mbovu, amezaliwa naye atazaa wake pia. Kwamba anayeonekana bora sana ameandaliwa vyema. Tusidharau asili yetu hata kidogo.

Learn languages from TV shows, movies, news, articles and more! Try LingQ for FREE